NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE AIPONGEZA REA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA NISHATI VIJIJINI


Na Mwandishi Wetu

DODOMA

NAIBU Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Mhe. Cosato Chumi aipongeza Wakala wa Nishati Vijijini(REA) namna  ilivyotekeleza Miradi mbalimbali vijijini na kuleta tija kwa wananchi.

Agosti 7,2025 Mh. Chumi alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la REA katika maonesho ya Wakulima Nanenane

Amesema Miradi yote inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekuwa na athari chanya kwenye maendeleo ya watu waishio vijijini.

“Nawapongeza REA kwa kazi nzuri na ufanisi katika kutekeleza Mradi wa Ujazilizi II (C) na Mradi wa Taa za Barabarani, Sisi Mafinga ni wanufaika wa Miradi ya REA.” Amefsfanua Mhe. Chumi.



Chapisha Maoni

0 Maoni