DODOMA
Mwenyekiti wa Bodi VETA Prof. Sefuni Ernest Mchome ameyasema hayo alipotembea banda hilo katika maonesho ya Wakulima Nanenane mkoani Dodoma.
Prof.Mchome amesema VETA inajukumu la kuhakikisha watanzania wa makundi mbalimbali wanapata elimu na mafunzo ya ufundi stadi ili mafunzo hayo yawasaidie katika maisha yao ya kila siku
Ameongeza kuwa Veta imepiga hatua kubwa katika ubunifu mbalimbali ambao unaoneshwa kwenye maonesho, kama bunifu zinazotimia nishati ya umeme, maji na nishati ya jua, na vifaa mbalimbali vinavyowasaidia wakulima kuvuta na kumwagilia inayotumia gharama ndogo
Amebainisha kuwa mwaka jana kulikua na bunifu wa kutumia mapanga ya kusukumwa na nguvu ya upepo lakini mwaka huu ubunifu umeongezeka wa kutumia nishati ya jua.
Amezitaja bunifu nyingine kuwa ni vifaa vya kutengeneza chakula cha kuku, samaki na mifugo kwa kuwa gharama yake ni ndogo na zinaweza kuleta manufaa katika shughuli zao

0 Maoni