SERIKALI KUHAKIKISHA SEKTA YA MADINI INAKUWA NA MCHANGO KATIKA UKUAJI WA UCHUMI

 


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa sekta ya madini inaendelea kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi wa nchi.

Dkt. Biteko amebainisha hayo leo Oktoba 25, 2023 akifungua Mkutano wa Kimataifa wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIF) wa Mwaka 2023 jijini Dar es Salaam.

“Mpango wa Serikali ni kuhakikisha kuwa Sekta hii inachangia asilimia 10 au zaidi katika pato la Taifa ifikapo 2025,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa mchango wa Sekta ya Madini umekuwa ukiongezeka kutoka asilimia 7.3 mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 9.1 mwaka 2022.

Kwamba ukuaji wa Sekta ya Madini kwa mwaka 2022 umekuwa asilimia 10.9 ukilinganishwa na ukuaji wa asilimia 9.4 mwaka 2021.

“Ni matumaini yetu Sote ifikapo mwaka 2025, Sekta ya Madini itafikia lengo la mchango wa asilimia 10 kwenye pato la Taifa,” amesema Dkt. Biteko na kuongeza,

“Mchango wa Sekta ya Madini katika fedha za kigeni kwa mauzo yote ya bidhaa nje ya nchi umeendelea kuimarika kutoka dola za Marekani 1.6 bilioni sawa na asilimia 37 mwaka 2018 hadi dola za Marekani 3.4 bilioni sawa na asimilia 47 mwaka 2022,”.

Chapisha Maoni

0 Maoni